Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Afrika imejiandaa kukabiliana na COVID-19 lakini yahitaji msaada:Dkt. Moet
Wakati janga la mlipuko wa virusi vya Corona au COVID-19 likiendelea kuitikisa dunia na kusababisha athari kubwa ikiwemo kupoteza maisha ya maelfu ya watu, bara la Afrika ambalo japo halina wagonjwa wengi linahitaji msaada ili kudhibiti kusambaa kwa virusi hivyo.
Ujuzi tulioupata wakati wa Ebola tutautumia kupambana na COVID-19-Wauguzi DRC
Wakati mlipuko wa ugonjwa Ebola ukielekea kufikia ukingoni nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC, wahudumu wa afya waliopata mafunzo wakati wa janga hilo, hivi sasa wanatumia ujuzi walioupata, kuimarisha mfumo wa afya nchini humo ikiwa na kutumia uwezo huo kupambana na virusi vya corona, COVID-19.
Hatua zaidi zachukuliwa kukabiliana na COVID-19 nchini Kenya
Kufuatia raia wa Kenya kulalamikia hatua ya Rais wa nchi hiyo kutangaza zuio la kusafiri katika baadhi ya mikoa kwa mfano kuingia jijini Nairobi, Msemaji wa serikali ya Kenya Cyrus Oguna ameieleza idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa kuwa tangazo hilo la rais Uhuru Kenyatta halina nia ya kumuumiza mtu yeyote bali kuwakinga wananchi wote dhidi ya virusi vya corona, COVID-19. Hadi sasa Kenya imethibitisha kuwa na wagonjwa 172 baada ya watu wengine 14 kugunduliwa kuwa na virusi hatari vya corona kwa muda wa saa 24 zilizopita. Jason Nyakundi ametuandalia makala hii akiwa mjini Nairobi.
UN na wadau Somalia watoa kipaumbele cha kukabiliana na COVID-19
Umoja wa Mataifa na washirika wake wa masuala ya kibinafdamu nchini Somalia wanaweka mipango na vipaumbele vipya ili kusaidia taifa hilo la Pembe ya Afrika katika maandalizi na hatua za kupambana na virusi vya Corona COVID-19.
Fikra za kikoloni katika kujaribu chanjo ya COVID-19 Afrika zikome- WHO
Mkurugenzi Mkuu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa Dkt. Tedros Ghebreyesus amesema ameshtushwa sana na kauli za wiki iliyopita kutoka kwa baadhi ya wanasayansi wakipendekeza kuwa majaribio ya kwanza ya chanjo dhidi ya ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19 yatafanyikia Afrika.
Asanteni wauguzi na wakunga na tuna deni kwenu – Guterres
Leo ni siku ya afya duniani ambapo ujumbe ukiwa ni saidia wauguzi na wakunga.
Tunahitaji kuwekeza haraka kuziba pengo la wauguzi duniani:WHO
Mlipuko wa virusi vya Corona COVID-19 unadhidhirisa haja ya kuimarisha jopo la wahudumu wa afya kote duniani , kwa mujibu wa ripoti mpya ya “hali ya wauguzi duniani 2020.”
COVIDI-19 yazua changamoto za kupata huduma za afya Uganda
Kuendelea kusambaa kwa virusi vya Corona, COVID-19 kumezifanya nchi kukaza uzi zaidi katika hatua za kukabiliana na mlipuko huo ikiwemo vikwazo vya watu kutembea na hatua za kuwataka kusalia majumbani. Vikwazo hivi pamoja na kusaidia kudhibiti mlipuko wa COVID-19 lakini pia vimezua changamoto zingine. Mathalani nchini Uganda ambako kuna marufuku ya watu kutembea wagonjwa wengi wameanza kupata changamoto ya kufikia huduma za afya kutokana na maagizo mapya yanayolenga kudhibiti kuenea kwa virusi hivyo kama alivyobaini mwandishi wetu nchini humo John Kibego katika makala hii
Mashabiki wa mpira wa miguu duniani kote tuunde timu moja dhidi ya COVID-19-WHO na FIFA
Shirikisho la soka ulimwewnguni FIFA limeungana na Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO katika kuunga mkono kampeni ya #BeActive yaani #Jishughulishe iliyozinduliwa leo katika Siku ya kimataifa ya Umoja wa Mataifa ya michezo kwa ajili ya maendeleo na amani ili kuhamasisha watu kuwa na afya wakiwa nyumbani wakati huu ambao dunia inaungana katika mapambano dhidi ya virusi vya corona, COVID-19, leo na kila siku.
Ubaguzi kwenye utoaji huduma dhidi ya COVID-19 utaleta janga zaidi- Wataalamu
Kikosi kazi cha waatalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu watu wenye asili ya Afrika, kimetaka kuwepo na uwiano na usawa wa makundi mbalimbali ya binadamu wakati wa utoaji wa huduma kwa wagonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19, la sivyo utoaji wa huduma kwa misingi ya rangi unaweza kusababisha vifo zaidi.