Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Picha ya juu ikionesha mtaa wa mabanda wa Mathare mjini Nairobi Kenya
UN-Habitat/Julius Mwelu

Maji ni muhimu ili makazi duni Kenya yadhibiti COVID-19

Lengo namba 6 la malengo ya maendeleo endelevu, SDG, linalenga kufanikisha upatikanaji wa maji kwa wote na kwa usawa ifikapo mwaka 2030. Lakini bado ulimwenguni kote, kama ripoti ya maendeleo ya maji ya Umoja wa Mataifa, ilivyoonesha, mabilioni ya watu bado wanakosa maji safi na salama na huduma za kujisafi na watu wanaachwa nyuma kwa sababu mbalimbali ikiwemo  ubaguzi kwa misingi ya jinsia, kabila, tamaduni na hali ya kijamii.
 

Chakula chenye virutubisho vya kutosha vya lishe kinaweza kumwondoa mtu hususani watoto katika hatari ya kupata magonjwa.
World Bank/Maria Fleischmann

Unafahamu nini kuhusu vyakula bora hususani wakati huu wa COVID-19?

Mwongozo uliotolewa na Shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO unasema japo lishe hutofautiana sana kutokana na mahali na kulingana na upatikanaji wa chakula, tabia za kula na tamaduni, lakini linapokuja suala la chakula, kuna mengi ambayo tunajua juu ya nini na nini sio nzuri kwetu na hii ni kweli bila kujali tunaishi wapi.

UN Photo/Martine Perret

Uzoefu tulioupata kukabiliana na ebola unatosha kukabiliana na COVID-19-muuguzi DRC

Wakati mlipuko wa ugonjwa Ebola ukielekea kufikia ukingoni nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC, wahudumu wa afya waliopata mafunzo wakati wa janga hilo, hivi sasa wanatumia ujuzi walioupata, kuimarisha mfumo wa afya nchini humo ikiwa  ni pamoja na kutumia uwezo huo kupambana na virusi vya corona, COVID-19 Grace Kaneiya na maelezo zaidi.
 
(Taarifa ya Grace Kaneiya)
 

Sauti
2'36"
Photo: WHO

Bara la Afrika japo halina wagonjwa wengi linahitaji msaada ili kudhibiti kusambaa kwa COVID-19-Dkt. Moeti

Wakati janga la mlipuko wa virusi vya Corona au COVID-19 likiendelea kuitikisa dunia na kusababisha athari kubwa ikiwemo kupoteza maisha ya maelfu ya watu bara la Afrika mabalo japo halina wagonjwa wengi linahitaji msaada ili kudhibiti kusambaa kwa virusi hiyo.
Hayo yameelezwa na mkurugenzi wa shirika la afya duniani WHO kanda ya Afrika Dkt. Matshidiso Moet akizungumza na Umoja wa Mataifa nakuongeza kwamba pamoja na changamoto zinazolikabili bara hilo  ambalo sasa limefikisha wagonjwa  zaidi 10,000 wa COVID-19, nchi zinajitahidi kufanya ziwezalo
(SAUTI YA DKT.MOET CUT 1)

Sauti
2'16"

8 Aprili 2020

Assumpta Massoi : Hujambo na Karibu kusikiliza Jarida kutoka Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa, kutoka hapa New York Marekani.

JINGLE (04”)

ASSUMPTA:Ni Jumatano 08 Aprili mwaka 2020, mwenyeji wako studioni hii leo ni mimi ASSUMPTA MASSOI

Sauti
12'13"