Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

04 JANUARI 2021

Katika Jarida la Habari za umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea

-Watu zaidi ya 100 wauawa katika shambulio kwenye jimbo la Tillaberi nchini Niger, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa alaani vikali shambulio hilo na kutaka wahusika wakamatwe na kuwajibishwa.

-Nchini Pakistan wachimba migodi ya makaa ya mawe 11 wameuawa katika shambulio la kigaidi lililotokea mwishoni mwa wiki kwenye jimbo la Balouchistan, watu wengine wengi wamejerihiwa na wengine kutekwa .

Sauti
10'6"