Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

UN News

Tuna njaa, ni maafa, asema mkimbizi wa Syria aliyeko Lebanon. UNHCR inajitahidi kusaidia. 

Ripoti hiyo ya Benki ya Dunia na UNHCR imechunguza madhara ya ugonjwa wa COVID-19 katika kuwasukuma wakimbizi wa Syria katika umaskini, wao pamoja na wenyeji wao nchini Jordan, Lebaon na aneo la Kurd nchini Iraq.  Ahimidiwe Olotu na taarifa zaidi.

Ripoti hiyo inasema watu wanaokadiriwa kufikia milioni 4.4 katika jamii wenyeji, na pia takribani wakimbizi milioni moja wa Syria, na Wairaq wengine 180,000 waliokimbia makazi yao wameanguka chini ya mstari wa umaskini tangu mwanzo wa janga la COVID-19. 

Sauti
2'36"