Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Yemi Alade: Niko tayari kujitolea kwa nguvu zangu zote kufanikisha malengo ya UNDP
Mwanamuziki Yemi Alade, raia wa Nigeria ambaye hivi karibuni ametangazwa kuwa Balozi mwema wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP amesema malengo ya UNDP yanaendana na malengo yake kwa hivyo atajitolea kwa uwezo wake wote. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.
Afrika, hatua tulizochukua dhidi ya COVID-19 zimedhihirishia ulimwengu uthabiti wetu.
Fikra za baadhi ya watu kuwa maelfu kwa maelfu ya watu barani Afrika watapukutika kutokana na janga la ugonjwa wa Corona, au COVID-19 zimekuwa ndivyo sivyo baada ya bara hilo kuchukua hatua kitaifa na kikanda na hatimaye hadi sasa kudhihirisha umuhimu wa mshikamano katika kukabili adui. Hilo limebainishwa wakati wa hotuba za marais waliohutubia mjadala mkuu wa mkutaon wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa njia ya mtandao kutokana na vikwazo vilivyopo Marekani kutokana na janga la Corona.
Hatua tulizochukua dhidi ya COVID-19 zimedhihirishia ulimwengu uthabiti wetu Afrika
Fikra za baadhi ya watu kuwa maelfu kwa maelfu ya watu barani Afrika watapukutika kutokana na janga la ugonjwa wa Corona, au COVID-19 zimekuwa ndivyo sivyo baada ya bara hilo kuchukua hatua kitaifa na kikanda na hatimaye hadi sasa kudhihirisha umuhimu wa mshikamano katika kukabili adui. Hilo limebainishwa wakati wa hotuba za marais waliohutubia mjadala mkuu wa mkutaon wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa njia ya mtandao kutokana na vikwazo vilivyopo Marekani kutokana na janga la Corona. Flora Nducha anamleta Assumpta Massoi ambaye amefuatilia hotuba za viongozi hao na anaeleza kwa kina.
Niko tayari kujitolea kwa nguvu zangu zote kufanikisha malengo ya UNDP-Yemi Alade
Mwanamuziki Yemi Alade, raia wa Nigeria ambaye hivi karibuni ametangazwa kuwa Balozi mwema wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP amesema malengo ya UNDP yanaendana na malengo yake kwa hivyo atajitolea kwa uwezo wake wote.