Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

© UNICEF/Frank Dejongh

Afrika, hatua tulizochukua dhidi ya COVID-19 zimedhihirishia ulimwengu uthabiti wetu.

Fikra za baadhi ya watu kuwa maelfu kwa maelfu ya watu barani Afrika watapukutika kutokana na janga la ugonjwa wa Corona, au COVID-19 zimekuwa ndivyo sivyo baada ya bara hilo kuchukua hatua kitaifa na kikanda na hatimaye hadi sasa kudhihirisha umuhimu wa mshikamano katika kukabili adui. Hilo limebainishwa wakati wa hotuba za marais waliohutubia mjadala mkuu wa mkutaon wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa njia ya mtandao kutokana na vikwazo vilivyopo Marekani kutokana na janga la Corona.

Sauti
6'4"
Mwanafunzi wa kike nchini Ghana akinawa mikono kwa sabuni kabla ya kurejea darasani ikiwa ni sehemu ya mpango wa serikali kuhakikisha elimu inaendelea huku wakidhibiti maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19.
UNICEF/Geoffrey Buta

Hatua tulizochukua dhidi ya COVID-19 zimedhihirishia ulimwengu uthabiti wetu Afrika 

Fikra za baadhi ya watu kuwa maelfu kwa maelfu ya watu barani Afrika watapukutika kutokana na janga la ugonjwa wa Corona, au COVID-19 zimekuwa ndivyo sivyo baada ya bara hilo kuchukua hatua kitaifa na kikanda na hatimaye hadi sasa kudhihirisha umuhimu wa mshikamano katika kukabili adui. Hilo limebainishwa wakati wa hotuba za marais waliohutubia mjadala mkuu wa mkutaon wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa njia ya mtandao kutokana na vikwazo vilivyopo Marekani kutokana na janga la Corona. Flora Nducha anamleta Assumpta Massoi ambaye amefuatilia hotuba za viongozi hao na anaeleza kwa kina.

Sauti
6'4"