Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
COVID-19 imenirudisha nyumbani kijijini-Waweru
Tangu lizuke janga la corona duniani athari nyingi za karibu kila sekta zimeshuhudiwa. Vijana ambao idadi yao ndiyo kubwa kwa karibu kila nchini duniani nao wameathirika pakubwa. Wengi walilazimika kusitisha masomo kufuatia kufungwa shule na taasisi za elimu, wengine wakapoteza ajira na kubaki katika hali ya sintofahamu kuhusu hatma ya maisha yao. Kijana Joseph Waweru alipoteza kibarua chake mjini Nairobi na pia mipango yake ya masomo katika chuo kikuu ikakwama ndipo akaamua kuhamia kwao alikozaliwa huko Kitale, magharibi mwa Kenya.
Nilipokuwa nakua, ukatili majumbani niliona jambo la kawaida, sasa hapana!
Livhuwani Hellen Dzibana, mshauri nasaha kutoka nchini Afrika Kusini, kutwa kucha hivi sasa anaomba janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 limalizike kwa kuwa limekuwa mwiba katika utekelezaji wa majukumu yake kwa ufasaha ya kusaidia manusura wa ukatili wa kingono, jambo ambalo analisimamia kidete baada ya kulitambua kwa kina. Kulikoni?
Livhuwani, mkazi huyu wa mji mkuu wa kibiashara wa Afrika Kusini, Johannesburg anasema kwamba katu wakati wa makuzi yake hakuwahi kufahamu maana ya ukatili wa kijinsia.
Janga la COVID-19 ni zaidi ya janga la kiafya, ni zahma ya kibinadamu:UN
Akizindua ripoti hiyo kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kwa njia ya mtandao Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema “hakuna nchi ambayo imenusurika, hakuna kundi la watu ambalo halijaguswa na gonjwa hilo na hakuna mtu aliye na kinga dhidi ya athari za janga hilo.” Jason Nyakundi na taarifa kwa kina.
16 Septemba 2020
COVID-19 ni zaidi ya janga la kiafya ni mzahma ya kibinadamu. Mshauri nasaha Afrika Kusini alalama COVID-19 kukwamisha kazi yake. Vita iliniondoa chuo kikuu kwetu Yemen, watu wa Jordan wamenipa fursa nyingine-Mkimbizi.
COVID-19 ni zaidi ya janga la kiafya, ni zahma ya kibinadamu:UN
Akizindua ripoti hiyo kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kwa njia ya mtandao Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema “hakuna nchi ambayo imenusurika, hakuna kundi la watu ambalo halijaguswa na gonjwa hilo na hakuna mtu aliye na kinga dhidi ya athari za janga hilo.”
Wakati nakua, ukatili majumbani niliona jambo la kawaida, sasa hapana!
Livhuwani Hellen Dzibana, mshauri nasaha kutoka nchini Afrika Kusini, kutwa kucha hivi sasa anaomba janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 limalizike kwa kuwa limekuwa mwiba katika utekelezaji wa majukumu yake kwa ufasaha ya kusaidia manusura wa ukatili wa kingono, jambo ambalo analisimamia kidete baada ya kulitambua kwa kina. Kulikoni?