Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Zaidi ya wahudumu wa afya 10,000 barani Afrika wameambukizwa COVID-19: WHO
Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO leo limeonya kuhusu tishio la janga la ugonjwa wa corona au COVID-19 kwa wahudumu wa afya barani Afrika.
Mustakbali wa wanafunzi wakimbizi wamulikwa kati ya changamoto ya COVID-19, Uganda
Baadhi ya hatua zilizochukuliwa na nchi nyingi duniani kama sehemu ya njia za kudhibiti kuenea kwa COVID-19, zimeathiri vibaya Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs likiwemo lile namba nne linalochagiza fursa za elimu bora. Nchini Uganda, kufungwa kwa taasisi za elimu ni miongoni mwa hatua za kwanza kabisa kuchukuliwa na hatimaye kuathiri moja kwa moja wanafunzi zaidi ya milioni 15. Hata hivyo serikali imetumia mbinu mbalimbali ikiwemo kusambaza masomo kupitia matangazo ya redio na televisheni ambavyo havijaweza kuwafikia wote.
Maskini walipwe kipato cha msingi kila mwezi kuepusha COVID-19- UNDP
Umoja wa Mataifa umesema kuwa kuwapatia watu maskini zaidi duniani kipato cha kujikimu, TBI, kunaweza kupunguza kasi ya kuenea kwa ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19.
Harakati za kupambana na COVID-19 zazidisha machungu kwa wayemen
Nchini Yemen, vita vya wenyewe kwa wenyewe na janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19, vimeleta taabu kwa wananchi huku familia zikihaha kujinusuru na Umoja wa Mataifa ukiingilia kati kusaidia. Assumpta Massoi anaarifu zaidi.
Hali si shwari nchini Yemen ambako hali ya upatikanaji wa afuta nao si mzuri, madereva katika mji mkuu, Sana’aa wakikesha kusubiri kununua mafuta na hata wakati mwingine baada ya kusubiri muda mrefu mafuta kumalizika kituoni.
Guterres: Ulimwengu wa Kiarabu ni wakati wa kugeuza janga la COVID-19 kuwa fursa
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameuambia ulimwengu wa nchi za Kiarabu kwamba sasa ni wakati wa kugeuza janga la virusi vya Corona au COVID-19 kuwa fursa ya kujijenga upya na kwa ubora zaidi. Jason Nyakundi na maelezo zaidi.
Guterres kupitia taarifa ya kisera kuhusu janga la COVID-19 na jinsi ya kujikwamua vyema katika nchi za ulimwengu aloyoitoa hii leo amesema janga hilo limedhihirisha mapungufu na hali tete katika jamii na uchumi duniani kote na ulimwengu wa Kiarabu haukusalimika.
23 JULAI 2020
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameuambia ulimwengu wa nchi za Kiarabu kwamba sasa ni wakati wa kugeuza janga la virusi vya Corona au COVID-19 kuwa fursa ya kujijenga upya na kwa ubora zaidi. Watoto zaidi ya 32 wamepoteza au kutenganishwa na mzazi mmoja au wote kutokana na Ebola tangu kuzuka kwa mlipuko mpya Juni Mosi kwenye jimbo la Equateur Magharibi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC,limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF. Nchini Yemen, vita vya wenyewe kwa wenyewe na janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19, vimeleta taabu kwa
Ulimwengu wa Kiarabu ni wakati wa kugeuza janga la COVID-19 kuwa fursa: Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameuambia ulimwengu wa nchi za Kiarabu kwamba sasa ni wakati wa kugeuza janga la virusi vya Corona au COVID-19 kuwa fursa ya kujijenga upya na kwa ubora zaidi.