Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Wafanyakazi wa maeneleo wakimkabidhi mwanamke msaada kufuatia janga la COVID-19 mjini Dhaka, Bangladesh
UN Women/Fahad Kaizer

COVID-19 inaweza kurudisha nyuma mafanikio yaliyofikiwa kwa miaka hata miongo-Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo akihutubia hafla ya uzinduzi wa “Mkutano wa juu wa Mawaziri la Siasa kuhusu Maendeleo Endelevu na Mkutano wa ngazi ya juu wa  Baraza la Uchumi na Jamii” ameeleza kuwa janga la COVID-19 linaweza kuyarejesha nyuma maendeleo yaliyofikiwa na  dunia kwa miaka kadhaa na hata miongo kadhaa na kuwa limeleta changamoto kubwa za kiuchumi na ukuaji katika nchi nyingi.