Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Msanii na mwanamuziki wa mtindo wa reggae Ziggy Marley alipoahidi kuunga mkono kampeni ya 'Sema ndio kwa watoto' alipotembelea Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Julai 2001
© UNICEF/Nicole Toutounji

Wimbo maarufu One Love wa Bob Marley kutengenezwa upya ili kuiunga mkono 'Reimagine' ya UNICEF

Wanafamilia wa mwanamuziki nguli na wa kukumbukwa sana duniani, Bob Marley, wametangaza kuutengeneza upya wimbo maarufu wa Bob Marley unaofahamika kwa jina One Love ili waunge mkono kazi za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto,  UNICEF, kurejesha tena ulimwengu wa haki zaidi kwa watoto ambao maisha yao yamevurugwa na janga la COVID-19, imeeleza taarifa ya UNICEF iliyotolewa hii leo mjini New York Marekani.