Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

© UNICEF

UNICEF yafikisha msaada wa COVID-19 kwa nchi zaidi ya 100 licha ya changamoto

Shirika la Umoja wa mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limesema licha ya changamoto lukuki limefanikiwa kufikisha msaada kwa nchi zaidi ya 100 kupambana na janga la corona au COVID-19 na kuokoa maisha ya mamilioni ya watu. 

Katika ripoti yake iliyotolewa leo mjini New York na Copenhagen, UNICEF imesema wakati janga la COVID-19 likipindua maisha ya mamilioni ya watoto kote duniani , UNICEF inafikisha msaada wa kuokoa maisha licha ya kukabiliwa na vikwazo vingi na vikubwa ikiwemo masuala ya usafiri na matatizo ya kiufundi.

Sauti
2'10"