Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Wanawake na watoto waliotawanywa kutokana na mapigano  Jebel Marra,  Darfur Kaskazini, wakijihifadhi katika kituo kipya cha Tawilla
OCHA

Sudan Kusini, Sudan, CAR, Libya na Haiti kunufaika na ufadhili wa OCHA/CERF

Taarifa iliyotolewa hii leo na ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia misaada ya dharura, OCHA imeeleza kuwa Mratibu Mkuu wa misaada ya dharura ya kibinadamu kwenye Umoja wa Mataifa ambaye pia ni mkuu wa, Mark Lowcock, hii leo ameachia dola za kimarekani milioni 25 kutoka mfumo mkuu wa dharura wa Umoja wa Mataifa, CERF kwenda kwa shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji, IOM ili kusaidia mashirika yasiyo ya kiserikali yaliyoko mstari wa mbele katika kutoa hudua ya afya ya kuokoa maisha, huduma za maji na za kujisafi katika mapambano dhidi ya COVID-19 katika Jamhuri ya Afrika ya kati, Haiti, Libya, Sudan Kusini na Sudan.