Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Meli zikiwa katika bandari ya Antwerp
Picha/ IMO

Mabaharia zaidi ya 150,000 wakwama melini sababu ya COVID-19:ILO

Mabaharia wanapaswa kuchukuliwa kama wafanyakazi muhimu hivyo wanastahili kuruhusiwa kurejea nyumbani -limesema leo shirika la kazi duniani ILO, wakati likitoa wito wa hatua za haraka za kuwaachilia mabaharia  kati ya 150,000 hadi 200,000 waliokwama kwenye meli kote duniani kwa sababu ya hatua za kukabiliana na janga la virusi vya corona au COVID-19.