Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Sindano imeandaliwa katika kituo cha umma  cha kampeni ya chanjo huko Sudani Kusini
UNMISS/Tim McKulka

Chanjo ni muhimu lakini pekee haitoshi:Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameuambia mkutano wa kimataifa kuhusu chanjo  unaofanyika leo kupitia njia ya mtandao kwamba chanjo ni muhimu sana na imeokoa maisha ya mamilioni ya watu duniani lakini peke yake haitoshi kukabiliana na majanga makubwa ya kiafya kama linaloisumbua dunia hivi sasa la COVID-19.

Sauti
2'11"