Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Tujikwamue vyema tukilinda bayoanuwai baada ya COVID-19: Guterres
Kujikwamua kutoka kwenye janga la virusi vya corona au COVID-19 kunapaswa kwenda sanjari nan chi kuungana katika kulinda maliasili ya dunia hii kwa mujibu wa ahadi za kimataifa kwa lengo la kufikia mustakabali bora kwa watu wote na sayari dunia, amesema leo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
Wanandoa wakumbana na karaha badala ya raha, kisa? COVID-19
Katika mada kwa kina leo tunaelekea Uganda, kumulika mizozo ya kifamilia wakati huu wa mlipuko wa COVID-19 na madhara yake. Mizozo ambayo inadaiwa kusababishwa na wanafamilia kukaa pamoja majumbani kwa muda mrefu kutokana na vizuizi vya kutembea vilivyowekwa na serikali ikiwa ni moja ya hatua za kudhibiti kuenea kwa virusi vya corona. John Kibego anatupatia picha halisi.
COVID-19 inaongeza madhila ya kibinadamu Yemen:OCHA
Yemen nchi iliyoathirika vibaya na vita vya wenyewe kwa wewe sasa imeachwa ikabiliane na janga la virusi vya corona au COVID-19 na mfumo wa afya ambao umesambaratika na bila usaidizi zaidi wa kifedha limeonya leo shirika la Umoja wa Mataifa la misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura OCHA.
Watu milioni 2.4 wahamishiwa kwenye makazi ya muda Bangladeshi kufuatia kimbunga Amphan
Kufuatia kimbunga Amphan kilichotua nchini Bangladesh wiki hii , wilaya 19 zimeathirika na watu zaidi ya milioni 2.4 wamelazimika kuhamishiwa kwenye makazi ya muda limesema leo shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP.
COVID-19 huenda ikawatumbukiza watoto wengine milioni 10 katika utapiamlo:WFP
Janga la virusi vya corona au COVID-19 huenda likawatumbukiza watoto wengine milioni 10 zaidi katika utapiamlo uliokithiri kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na shirika la mpango wa chakula duniani WFP.