Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Kambini Dadaab
UNHCR

COVID-19 yaingia katika kambi ya Dadaab, Kenya na UNHCR zaimarisha huduma ya afya katika kambi za wakimbizi

Baada ya wagonjwa wawili wa virusi vya corona kuthibitishwa katika kambi ya wakimbizi ya Dadaab nchini Kenya, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR hii leo limetoa taarifa kuwa kwa kushirikiana na mashirika mengine ya kutoa msaada wa kibinadamu pamoja na serikali ya Kenya wanaimarisha mapambano yao dhidi ya COVID-19 katika kambi za wakimbizi nchini humo.

Sauti
2'45"