Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
COVID-19 imeathiri wafanyakazi katika kila nyanja:ILO
Takwimu mpya zilizotolewa leo na shirika la kazi duniani ILO kuhusu athari za virusi vya corona au COVID-19 katika soko la ajira zinaonyesha kuna athari kubwa na mbaya kwa wafanyakazi wa sekta zisizorasmi za kiuchumi na kwa mamilioni ya makampuni duniani.
29 APRILI 2020
Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea
-Mashirika ya Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na la mpango wa chakula WFP yataka serikali kuchukua hatua kuepusha janga la njaa hasa baada ya watoto milioni 370 kukosa mlo shuleni kutokana na janga la virusi vya corona au COVID-19
-Kambini Dadaab nchini Kenya waalimu watumia Radio kutoa elimu kwa maelfu ya watoto waliolazimika kusalia nyumbani kutokana na janga la corona
COVID-19 si ukomo wa masomo kwa wakimbizi
Nchini Kenya matangazo ya shule kwa njia ya redio sasa yameanza katika kambi za wakimbizi ambapo walimu wanafundisha masomo kupitia redio za jamii ili wanafunzi waendelee na masomo hata wakati huu wa kusalia nyumbani kutokana na janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19.
Hatma ya watoto milioni 370 iko njia panda kisa? COVID 19:UNICEF/WFP
Mustakbali wa watoto milioni 370 uko njiapanda kwa sababu ya janga la virusi vya corona au COVID-19 lililosababisha kufungwa kwa shule zilizokuwa mkombozi wa lishe yao imesema taarifa ya mashirika ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo.