Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Unyanyapaa ni changamoto kubwa katika vita dhidi ya COVID-19 Uganda
Suala la unyanyapaa wa aina yoyote ile ni mtihani mkubwa katika jamii kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa ambao hutoa wito kila uchao kuhakikisha changamoto hiyo inatokomezwa .Wakati huu wa mlipuko wa janga la virusi vya Corona au COVID-19 unyanyapaa umeelezwa kujitokeza na kusababisha changamoto kwa wagonjwa na washukiwa na hata kuwafanya wengine kutojitokeza kufanya vipimo hali ambayo shirika la afya ulimwenguni WHO limeonya kuwa ni hatari kubwa na kikwazo cha kupambana na ugonjwa huo.
24 APRILI 2020
Katika Jarida la Habari hii leo Flora Nducha anakuletea
-Mwezi mtukufu wa Ramadhani unaanza leo kote duniani Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa awatakia kila la heri Waislam wote na kusema kwamba COVID-19 itaifanya Ramadhan ya mwaka huu kuwa tofauti kabisa
-Kamishina Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Michelle Bachelet amesema anatiwa hofu na kamatakamata na kubanwa kwa vyombo vya habari wakati huu wa janga la COVID-19 ambapo taarifa sahihi ni muhimu sana
Ushirikiano wa kimataifa wazinduliwa kufanya chanjo na tiba ya COVID-19 kupatikana kwa wote
Mkakati mpya wa kimataifa umezinduliwa leo ili kusongesha mbele juhudi za maendeleo, uzalishaji na fursa sawa ya nyenzo mpya za kukabiliana na janga la virusi vya corona au COVID-19 hasa katika upatikanaji wa chanjo.
Mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani mwaka huu ni tofauti kabisa- Guterres
Waumini wa dini ya kiislamu ulimwenguni wakianza kufunga mwezi mtukufu wa Ramadhani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa ujumbe wake wa kuwatakia heri katika mfungo wa sasa ambao amesema ni tofauti kabisa na mingine iliyotangulia kwa ajili ya janga la COVID-19.
Kwa kila siku inayopita, athari za janga la COVID-19 na matokeo yake ni dhahiri :UNFPA
Kwa kila siku inayopita, athariza janga la COVID-19 na matokeo yake ni dhahiri :UNFPA
Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu duniani UNFPA , limesema linashikamana na wale wote wanaojitolea na kuwa katika mstari wa mbele kupigana na janga la virusi vya corona au COVID-19: kuanzia kwa wahudumu wa afya na wanaojitolea kusaidia bila malipo.