Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Kutoka kupanga safari za ndege hadi kusambaza vifurushi vya mlo; UNWTO yachukua hatua
Shirika la utalii la Umoja wa mataifa, UNWTO, limetoa mapendekezo ya kusaidia sekta ya utalii wakati huu ambapo ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 umetikisa sekta hiyo kote ulimwenguni.
Ulinzi wa amani: Kuanzia kusaidia nchi kuondoka katika migogoro, na sasa COVID-19
Kama ilivyo kwingine kote duniani, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanakabiliana na changamoto zinazoletwa na mlipuko wa virusi vya corona, COVID-19. Lakini kazi yao inaendelea na wanaendelea kutekeleza majukumu yao muhimu ya amani na usalama.
Ni wakati wa kugeuza maneno kuwa vitendo kusitisha uhasama:UN
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema wito wake wa kimataifa alioutoa wiki iliyopita wa kusitisha uhasama umepokelewa vyema kote duniani lakini ameonya kwamba kuna pengo kubwa kati ya azma na uteekelezaji na kusisitiza kwamba ili kunyamazisha silaha ni lazima kupaza sauti kwa ajili ya amani na kugeuza maneno kuwa vitendo.
Hospitali ya taifa Tanzania, Muhimbili yatenga sehemu maalum kwa ajili ya kunawa mikono
Tanzania kama ilivyo katika mataifa mengine imeweka mikakati kwa ajili ya kudhibiti kuenea kwa virusi vya corona au COVID-19. Hatua mbali mbali zinachukuliwa na serikali na pia mashirika binafsi yanaunga mkono juhudi za serikali. Afisa wa maswasiliano wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa jijini Dar es Saalam, UNIC ametembelea hospital ya taifa ya Muhimbili kushuhudia baadhi ya mikakati iliyowekwa kama sehemu ya juhudi za kudhibiti kuenea kwa virusi hivyo
Hatua za kupambana na COVID-19 Sudan zaathiri misaada ya kibinadamu:OCHA
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada ya kibinadamu OCHA leo limesema hatua za kupambana na kusambaa kwa virusi vya Corona , COVID-19 zinaathiri fursa, ufikishaji wa misaada na huduma za kibinadamu nchini Sudan.
Licha ya kufuta maadhimisho sababu ya COVID-19 mabomu ya kutegwa ardhini bado tishio:UN
Umoja wa Mataifa umesema pamoja na hatua kubwa zilizopatikana katika kukabiliana na mabomu ya kutegwa ardhibni kote duniani , mabomu hayo bado ni tishio kubwa .