Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Ni nani anawalinda watu wenye ulemavu dhidi ya COVID-19?-Mtaalamu wa UN
Mtaalamu maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wenye ulemavu, Catalina Devandas, hii leo mjini Geneva ameonya kwamba juhudi kidogo sana zimefanywa kuwapa maelekezo na usaidizi unaohitajika, watu wenye ulemavu ili kuwalinda wakati wa mlipuko huu wa ugonjwa wa COVID-19 ingawa wengi wao wako katika kundi la wale walioko hatarini zaidi.
Nchi za Kusini Mashariki mwa Asia ongezeni vita dhidi ya COVID-19:WHO
Wakati nchini za Kusini Mashariki mwa asia zikiripoti visa zaidi ya 480 wa virusi vya Corona COVID-19 na vifo 8, shirika la afya ulimwenguni WHO leo limetoa wito kwa nchi hizo kuchukua hatua sasa na kuongeza juhudi haraka kukabiliana na ugonjwa huo.
China yadhihirisha COVID-19 inaweza kudhibitiwa
Uzoefu wa China katika kudhibiti kusambaa kwa virusi vya Corona unaweza kutumika kama somo kwa nchi zingine ambazo sasa zinakabiliwa na mlipuko huo wa COVID-19 amesema afisa wa shirika la afya ulimwenguni WHO nchini China.
COVID-19 kuathiri elimu ya mamilioni ya watoto duniani kote
Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO limesema nchi 100 duniani zimefunga kabisa au kwa kiasi fulani shule na vituo vya elimu na kuwakoseha mamilioni ya watoto masomo, kwa sababu ya mlipuko wa COVID-19 unaoendelea. Grace Kaneiya na taarifa zaidi
(TAARIFA YA GRACE)
Shirika hilo sasa linasema hivi sasa linazisaidia nchi kusala suluhu ya jinsi ya Watoto kuweza kusoma wakiwa nje ya mazingira ya shule ikiwemo kupitia mtandaoni na nyenzo zingine za kidijitali
Watoto milioni 776 wakosa kuhudhuria shule kwa sababu ya COVID-19:UNESCO
Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO limesema nchi 100 duniani zimefunga kabisa au kwa kiasi fulani shule na vituo vya elimu na kuwakosesha mamilioni ya watoto masomo, kwa sababu ya mlipuko wa COVID-19 unaoendelea.
COVID-19: Shule Tanzania zafungwa mikusanyiko isiyo ya lazima marufuku
Kufuatia kubainika kwa mgonjwa wa virusi vya Corona nchini Tanzania, taifa hilo la Afrika Mashariki limeanza kuchukua hatua kuepusha maambukizi zaidi ambapo hii leo limetangaza hatua kadhaa ikiwemo kufungwa kwa shule zote za awali, za msingi hadi sekondari kwa siku 30 kuanzia leo.