Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Kituo cha udhibiti wa magonjwa, CDC, nchini  Marekani kimeanza operesheni zake za dharura kusaidia wadau wa afya katika kukabiliana na mlipuko wa virusi vya Corona duniani.
CDC/James Gathany

Corona isituchanganye, tuchukue hatua; Syria nako ni janga linalotia shaka zaidi- Guterres

Makombora yakizidi kumiminikia raia wasio na hatia nchini Syria, huku virusi vya Corona navyo vikizidi kusambaa maeneo mbalimbali duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amezungumza na waandishi wa habari na kuhusu zahma hizo akisema  kuwa kwa Corona huu si wakati wa kuchanganyikiwa na kwa Syria, janga hilo ni moja ya mazingira ya kutia shaka zaidi kwenye muongo wa sasa.