Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Watu wakiwa wamevaa barakoa kujikinga na virusi vya Corona. Hapa ni uwanja wa  ndege wa kimataifa wa Narita jijini Tokyo, Japan
UN News/Li Zhang

Virusi vya Corona na utalii; UNTWO yapaza sauti

Wakati virusi vya Corona, COVID-19 vikiendelea kuibua sintofahamu duniani hivi sasa, shirika la utalii la Umoja wa Mataiaf, UNWTO limesema linashirikiana na shirika la afya ulimwenguni, WHO na wadau wengine kusaidia mataifa kutekeleza mikakati ya kupunguza rabsha zisizo za lazima katika safari na biashara za kimataifa.