Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Pata habari kuhusu matumizi ya Akili Mnemba

Nyani wawili wekundu wa aina ya mbega wako katika msitu wenye majani mengi katika Msitu wa Jozani, Zanzibar, Tanzania.
UNDP Tanzania/Kumi Media

Fahamu programu ya JozaniAI, inayotumiwa Zanzibar kuboresha huduma za utalii

Programu ya JozaniAI, imeandaliwa kwa ushirikiano na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, UNDP nchini Tanzania ambapo Naibu Mwakilishi wake, John Rutere akizungumza na Idhaa ya Kiswahili ya UN amesema tayari imeleta manufaa makubwa katika kutatua changamoto. Apu hiyo imepatiwa jina kutoka hifadhi pekee ya taifa visiwani humo, Jozani, iliyosheheni vivutio lukuki wakiwemo kima punju na misitu ya mikoko.