Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkutano wa 4 wa Kimataifa kuhusu Ufadhili kwa Maendeleo

Mkutano wa 4 wa Kimataifa wa Ufadhili kwa Maendeleo
30 Juni - 3 Julai, Sevilla, Hispania

Karibu kwenye matangazo maalum ya Habari za UN kuhusu Mkutano wa Nne wa Kimataifa wa Ufadhili kwa Maendeleo (FFD4), unaofanyika Sevilla, Hispania.

Mkutano huu wa kihistoria unawakutanisha viongozi wa dunia, taasisi za kimataifa, sekta ya biashara, asasi za kiraia na mfumo wa Umoja wa Mataifa ili kukabiliana na changamoto za dharura za kifedha zinazokwamisha maendeleo ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).

FFD4 unatoa fursa muhimu ya kubadili mazingira ya kifedha duniani na kuhamasisha rasilimali zinazohitajika kwa ajili ya siku za usoni zenye usawa na endelevu zaidi.

Endelea kuwa nasi kwa taarifa za moja kwa moja, maoni ya wataalamu, na taarifa za kina kutoka Sevilla.

Iftin na Aminaa wakiwa wamesimama mbele ya taa za barabarani zinazotumia nishati ya sola, ambazo sasa zinawezesha wasichana kutembea bila  hofu nyakati za usiku wakitoka masomoni.
© IOM/Spotlight Communications

IOM yawezesha maendeleo yanayoongozwa na jamii nchini Somalia

Jumuiya ya kimataifa ikijiandaa kukutana Hispania kujadili Ufadhili kwa Maendeleo duniani, tunakuletea simulizi ya ustahimilivu kutoka Somalia ambayo ni kumbusho tosha la manufaa ya mbinu bunifu za ufadhili. Katika Jimbo la Galmudug, katikati mwa Somalia, ndoto ya wasichana wawili, Iftin na Aminaa  ya kujiunga na Chuo Kikuu mjini Abudwaq ilikumbwa na changamoto nyingi.