Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkutano wa 4 wa Kimataifa kuhusu Ufadhili kwa Maendeleo

Mkutano wa 4 wa Kimataifa wa Ufadhili kwa Maendeleo
30 Juni - 3 Julai, Sevilla, Hispania

Karibu kwenye matangazo maalum ya Habari za UN kuhusu Mkutano wa Nne wa Kimataifa wa Ufadhili kwa Maendeleo (FFD4), unaofanyika Sevilla, Hispania.

Mkutano huu wa kihistoria unawakutanisha viongozi wa dunia, taasisi za kimataifa, sekta ya biashara, asasi za kiraia na mfumo wa Umoja wa Mataifa ili kukabiliana na changamoto za dharura za kifedha zinazokwamisha maendeleo ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).

FFD4 unatoa fursa muhimu ya kubadili mazingira ya kifedha duniani na kuhamasisha rasilimali zinazohitajika kwa ajili ya siku za usoni zenye usawa na endelevu zaidi.

Endelea kuwa nasi kwa taarifa za moja kwa moja, maoni ya wataalamu, na taarifa za kina kutoka Sevilla.

03 JULAI 2025

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayokupeleka nchini Uganda katika Mbuga ya Wanyama inayofahamika kwa jina Murchison Falls National Park kuangazia namna washiriki wa Kongamano la kimataifa la lugha ya Kiswahili lililofanyika mapema mwaka huu jijini Kampala walivyofurahia mazigira asili nchini Uganda na namna yanavyounufaisha ulimwengu.

Sauti
9'58"
UN News/Matt Wells

IOM yasema uwekezaji wa kibunifu katika uhamiaji ni muhimu

Katika Mkutano wa nne wa kimataifa wa Ufadhili wa Maendeleo (FFD4) unaoendelea jijini Seville, Hispania, Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) limetoa wito wa kuimarisha uwekezaji wa kibunifu katika uhamiaji wa watu ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kusaidia kuziba pengo la kila mwaka la dola trilioni 4 za ufadhili wa maendeleo. Anold Kayanda anaeleza zaidi.

Sauti
1'59"

02 JULAI 2025

Hii leo jaridani tunaangazia wahamiaji na njia bunifu ya kuwawezesha kujikimu kimaisha, na malezi bora ya watoto nchini Tanzania. Makala tunasalia huko huko Tanzania kumulika uwekezaji na ufadhili wa miradi ya maendeleo, na mashinani tunakwenda nchini Kenya.

Sauti
9'59"
Waandishi wa habari wanafanya kazi katika kituo cha vyombo vya habari cha mkutano wa FFD4 huko Sevilla, Uhispania.
UN News/Matt Wells

IOM yataka uwekezaji wa kibunifu katika uhamiaji

Katika Mkutano wa nne wa kimataifa wa Ufadhili wa Maendeleo (FFD4) unaoendelea jijini Seville, Hispania, Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) limetoa wito wa kuimarisha uwekezaji wa kibunifu katika uhamiaji wa watu ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kusaidia kuziba pengo la kila mwaka la dola trilioni 4 za ufadhili wa maendeleo.

Sauti
1'59"

01 JULAI 2025

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kumulika ukame na uhakika wa upatikanaji wa maji na kusikia jinsi taifa la Chile, linatumia sera kushawishi mabadiliko yanayoweza kukabiliana na tatizo hilo. Pia tunakuletea muhtasari na mashinani.

Sauti
9'59"
UN Photo/Manuel Elías

Guterres awaambia viongozi wa dunia huko Sevilla Ni wakati wa kufadhili mustakabali wetu na kubadilisha mwelekeo

Mkutano  wa 4 wa ufadhili kwa ajili ya maendeleo FFD4 umeng’oa nanga rasmi leo huko Selilla Hispania kwa wito wa kuziba pengo la ufadhili wa maendeleo ili kutimiza ahadi ya kimataifa ya kutomwacha yeyote nyumba. Mkutano huo uliowaleta pamoja washiriki 2,500 kutoka nchi 150 wakiwemo wakuu wa nhi 50 na wadau wengine unasema kuna pengo la dola trilioni 4 katika ufadhili wa maendeleo linalohitaji kuzibwa. Anold Kayanda amefuatilia na anatupasha zaidi

Sauti
2'45"

30 JUNI 2025

Hii leo jaridani tunaangazia mkutano wa 4 wa ufadhili kwa ajili ya maendeleo FFD4 huko Sevilla Hispania, na siku ya Mabunge tukizungumza na mmoja wao kutoka Tanzania. Makala inatupeleka nchi Kenya na mashinani tunarejea huko huko Tanzania, kulikoni?

Sauti
11'41"