Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Chini ya nusu ya Nchi Zilizoendelea na chini ya theluthi moja pekee ya Nchi Zinazoendelea za Visiwa Vidogo zina mfumo wa maonyo ya mapema.
© UNDRR/Amir Jina

Nchi zilizo katika bonde la mto Nile kunufaika na mradi wa tahadhari za mapema

Maji yakiwa mengi yanaweza kusababisha mafuriko kama yaliyotokea hivi karibuni huko nchini Libya na uwepo wa maji kidogo unaweza kusababisha ukame kama hali ilivyo kwa nchi nyingi za ukanda wa Jangwa la Sahara kwa sasa, na ndio maana wadau wa masuala ya hali ya hewa wametaka suala la maji kuwa kitovu wakati dunia inashughulikia mabadiliko ya tabianchi.