Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
UNCTAD limesema mwaka 2022 umekuwa mgumu ukiziacha familia nyingi zikihaha kuweka mlo mezani
Kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo UNCTAD imesema mwaka huu wa 2022 umekuwa mgumu sana ambapo familia nyingi zimekuwa zikihaha kuweka mlo mezani na kujikimu hadi mwisho wa mwezi, lakini kuna suluhu na suluhu hizo zinapaswa kuwa za kimkakati na za kimataifa.
Kauli hiyo ni kwa mujibu wa Rebeca Grynspan katibu mkuu wa UNCTAD akihojiwa katika kipindi maalum cha UNCTAD Tradecast kuhusu kumalizika mwaka huu wa 2022 na kinachotarajiwa mwakani.
Mwaka 2022 umekuwa mgumu ukiziacha familia nyingi zikihaha kuweka mlo mezani: UNCTAD
Kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo UNCTAD imesema mwaka huu wa 2022 umekuwa mgumu sana ambapo familia nyingi zimekuwa zikihaha kuweka mlo mezani na kujikimu hadi mwisho wa mwezi, lakini kuna suluhu na suluhu hizo zinapaswa kuwa za kimkakati na za kimataifa.
Athari za ukame Pembe ya Afrika, WHO na wadau waingilia kati kupambana na utapiamlo mkali
Karomoja, moja ya mikoa nchini Uganda, kaskazini mashariki mwa nchi, Uganda inakopakana na Sudan na Kenya kama ilivyo kwa maeneo mengine katika ukanda huo wa Pembe ya Afrika, nako kumeathiriwa na ukame mkali na hivyo kuyumbisha upatikanaji wa chakula.