Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Wakuu wa UNHCR, Filippo Grandi (wa pili kulia), na IOM, António Vitorino (wa pili kushoto), wakitembelea kituo cha misaada ya kibinadamu cha UNHCR huko Agadez, katikati mwa Niger.
© UNHCR/Colin Delfosse

Wahamiaji ni msingi wa maendeleo toka enzi na enzi, tusiwabague bali tuwasaidie: IOM

Katika kuelekea siku ya kimataifa ya wahamiaji duniani itakayoadhimishwa tarehe 18 desemba mwaka huu, shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM limemtaka kila mtu atafakari, mhamiaji ni nani? mchango wa wahamiaji na endapo hapa duniani kuna mtu yeyote ambaye hajawahi kufikiria kuondoka aliko na kwenda kusaka mustakhbali bora, kwani  hatua hii itasaidia kutambua sababu ya uhamiaji na mchango wake kwenye jamii ambako wanakwenda.

Sauti
2'29"