Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
COP27: Unachohitaji kufahamu kuhusu mkutano mkubwa wa Mabadiliko ya Tabianchi wa Umoja wa Mataifa la mwaka huu.
Mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa mkataba wa Kimataifa wa tabianchi COP27 mwaka huu unafanyika huko Sharm el-Sheikh,nchini Misri wakati ambapo dunia inashuhudia ongezeko la hali mbaya ya hewa duniani kote, shida ya nishati iliyochochewa na vita vya Ukraine, na takwimu za wanasayansi zinasisitiza kwamba ulimwengu haufanyi vya kutosha kukabiliana na utoaji wa hewa ya kaboni na kulinda mustakabali wa sayari yetu.
Ufadhili zaidi unahitajika kwa ajili ya kujenga mnepo dhidi ya mabadiliko ya tabianchi:UNEP
Nchi lazima zichukue hatua haraka ili kukabiliana na athari za sasa na zijazo za mabadiliko ya tabianchi, kwani juhudi za sasa ni ndogo sana nana zinafanyika polepole mno, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa mazingira (UNEP) katika ripoti yake iliyochapishwa leo.
Mabadiliko ya tabianchi yazidisha zahma ya utapiamlo na njaa Sudan Kusini:UNICEF/FAO/WFP
Umoja wa Mataifa umeonya hii leo kuwa njaa na utapiamlo vinaongezeka katika maeneo yote yaliyokumbwa na mafuriko, ukame na mizozo nchini Sudan Kusini huku baadhi ya jamii zikiwa hatarini kukumbwa na njaa iwapo misaada ya kibinadamu haitakuwa endelevu, halikadhalika mikakati ya kukabili madhara ya mabadiliko ya tabianchi haitaimarishwa.