Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Makamu wa Rais wa Sudan Kusini Hussein Abdelbagi Akol Agany akihutubia mjadala wa wazi wa Baraza Kuu UNGA77
UN Photo/Cia Pak

Amani inaimarika Sudan Kusini lakini bado tuna changamoto: Agany

Amani nchini Sudan Kusini inaendelea kuimarika huku idadi kubwa ya wakimbizi wa ndani wameanza kurejea katika makazi yao kwenye maeneo ambako utulivu umerejea na serikali inafanya kila iwezalo kuhakikisha mkataba wa amani unadumiswa amesema makamu wa Rais wa Sudan Kusini Hussein Abdelbagi Akol Agany akihutubia mjadala wa wazi wa Baraza kuu hii leo mjini New York Marekani.

Rais wa Comorrow Azali Assoumani akihutubia mjadala wa Baraza Kuu
UN Photo/Cia Pak

Vita ya Ukraine imetuletea adha dunia nzima: Azali Assoumani

Rais wa kisiwa cha Comoro Azali Assoumani akihutubia mjadala wa wazi wa Baraza Kuu kikao cha 77 amesema jumuiya ya kimataifa hivi sasa inakabiliwa na changamoto lukuki, kuanzia athari za kiafya kama janga la COVID-19 ambalo linaingia mwaka wa tatu ssasa, mabadiliko ya tabianchi hadi vita ya Ukraine ambayo imeleta adha kwa dunia nzima.