Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

07 SEPTEMBA 2022

Katika jarida la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea 

-Katibu Mkuu UN atoa wito kwa ushirikiano wa kimataifa kukabiliana na uchafuzi wa hali ya hewa katika siku ya kimataifa ya hewa safi kwa ajili ya anga ya bluu

-Hatuwezi kusubiri hadi baa la njaa litangazwe Somalia tunafanya kila tuwezalo kuwanusuru Wasomali limesema shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP 

Sauti
12'18"