Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres (katikati) akutana na wanachama wa vyama vya ushirika vya kilimo vinavyoongozwa na wanawake na wanaume wazawa katika Kijiji cha Pierre Kondre-Redi Doti, katika ukanda wa msitu wa kitropiki wa Suriname.
UN Photo/Evan Schneider

Suriname inatoa “tumaini na msukumo kwa ulimwengu kuokoa misitu yetu ya mvua”: Mkuu wa UN

Suriname inaweza kuwa nchi ndogo na isiyo na watu wengi zaidi katika ukanda wa  Amerika ya Kusini, lakini ni moja ya nchi za kijani kibichi. Inachukuliwa kuwa kinara wa kimataifa katika uhifadhi wa bioanuwai, huku zaidi ya asilimia 90 ya ardhi yake ikifunikwa na misitu ya asili, rasilimali asilia isiyo na kifani ya taifa zaidi ya kufidia saizi yake.