Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Wavuvi pwani ya Kenya.
UN News/Thelma Mwadzaya

Tusipoilinda bahari tunaathiri kizazi cha sasa na vijavyo: Wananchi wa Vanga Kenya 

Ikiwa leo ni siku ya bahari duniani Umoja wa Mataifa imeichagiza dunia kuchukua hatua Madhubuti ili kuhakikishwa inalindwa kwa ajili ya maslhai ya kizazi cha sasa na kijacho kwani bahari sio tu inahakikisha uhakika wa chakula kwa mamilioni ya watu , bali pia ni moja wa muajiri mkubwa na inachangia kwa kiasi kikubwa katika pato la dunia la kila mwaka.