Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Majanga ikiwemo mabadiliko ya hali ya hewa inasababisha watu kukimbiz makwao.
© UNFPA Ethiopia/Paula Seijo

Zaidi ya watu milioni 30 walifungasha virago 2020 kutokana na majanga:UNDRR

Zaidi ya watu milioni 30 walikimbia makazi yao kutokana na majanga mwaka 2020 pekee, na idadi hii huenda ikaongezeka kutokana na kuongezeka kwa hatari na idadi ya matukio makubwa yanayohusiana na hali ya hewa. Jopo katika Kikao cha 7 cha Jukwaa la Kimataifa la Kupunguza Hatari za majanga (GPDR2022), lililosimamiwa na Sarah Charles, Msimamizi Msaidizi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani, limeangazia mbinu za kuimarisha utawala ili kupunguza hatari za majanga ya kuhamishwa.