Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Mamia ya maelfu ya watu wamefurushwa kaskazini-mashariki mwa Nigeria.
UNOCHA/Damilola Onafuwa

Lazima tutambue changamoto za Kaskazini mwa Nigeria ili tuweze kuleta matumaini:Guterres 

Changamoto kubwa zinazokabili jimbo la kaskazini mashariki mwa Nigeria la Borno, ambazo ni pamoja na ugaidi, zinahitaji kutambuliwa na jumuiya ya kimataifa ili kuunda kile ambacho Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amekiita "hali ya matumaini na hali halisi," katika eneo ambalo amesema halikufikia kilele cha sifa yake ya ugaidi, vurugu, kufurusha watu makwao au kukata tamaa.