Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

07 Aprili 2022

Ungana na Leah Mushi anayekuletea jarida hii leo likianza na maadhimisho ya siku ya afya, WHO imetoa wito kwa serikali na wananchi kwa ujumla kutunza mazingira. 

Leo pia ni siku ya kumbukizi ya mauaji ya Kimbari ya Rwanda dhidi ya watutsi ya mwaka 1994 hayakuwa ya bahati mbaya ya yalikuwa yanaweza kuzuilika. 

pia utasikia kuhusu walinda amani wa Tanzania waliotembelea wafungwa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, Makala kutoka Zambia kuhusu ardhi oevu na ujumbe kwa watu kuendesha baiskeli kwa ajili ya kulinda afya zao. 

Karibu usikilize. 

Sauti
12'28"