Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Nchini Madagaska, Rachelle Elien, afisa wa masuala ya kibinadamu wa OCHA na mwanachama wa timu ya dharura ya UNDAC, hukutana na watu walioathirika baada ya Kimbunga cha Emnati.
Chris Monnon / Atlas Logistique / OCHA

Kimbunga Emnati kuongeza zahma Madagascar:WFP

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP limesema kimbunga Emnati kilichoikumba Madagascar Jumatano ya wiki hii (23/02/2022) kikiwa kimbunga cha nne kulikumba taifa hilo katika wiki kadhaa kinatishia uhakika wa chakula na ni mfano wa kjinsi gani cangamoto za mabadiliko ya tabianchi zisiposhughulikiwa zinaweza kusababisha mahitaji makubwa ya kibinadamu.