Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Basi la National Express lisilotoa hewa chafuzi likiwa nje ya Mkutano wa mabadiliko ya tabianchi COP26 huko Glasgow, Scotland.
UN News/Laura Quinones

Wakati umefika kugeukia usafiri unaolinda mazingira: COP26

Kuwa na dunia ambayo vyombo vya usafiri kama magari, mabasi na malori ambayo yanatumia umeme n ani ya gharama nafuu, kuwa dunia ambayo vyombo wa usafiri wa bahari vinatumia nishati safi pekee na ndege ziweze kusafiri kwa kutumia hewa safi ya Hydrogen inaweza kuonekana kama ndoto ama sinema lakini kwenye mkutano wa COP26 unaoendelea huko Glasgow serikali nyingi na makampuni ya biashara wamesema wameanza kutimiza ndoto hizi na kuzifanya kuwa hali halisi. 

10 Novemba 2021

Hii leo katika jarida tunakueletea mada kwa kina mahsusi kutoka nchini Tanzania ikiangazia mchango wa vijana na ubunifu wa matumizi ya mifumo ya mawasiliano na teknolojia katika kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs.

Pia utasikia habari kwa ufupi ambao ripoti mbili zimetolewa hii leo na mashirika ya Umoja wa Mataifa moja ikiangazia masuala ya chakula na nyingine ikiangazia watoto wenye ulemavu duniani.

Sauti
12'20"