Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu
09 Novemba 2021
Karibu kusikiliza jarida ambapo miongoni mwa taarifa utakazo sikia leo ni pamoja na:-
Mlinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Nepal Sangya Malla anayehudumu katika ujumbe wa Umoja huo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo -DRC, MONUSCO ameshinda tuzo ya Afisa Polisi Mwanamke wa Umoja wa Mataifa kwa mwaka 2021
Wakulima wanabeba gharama kubwa ya mabadiliko ya tabianchi Bangladesh:IFAD
Nchini Bangladesh mabadiliko ya tabianchi yamekuwa ni mwiba kwa maisha ya kila siku ya watu wa taifa hilo la Asia. Kwa mujibu wa mfuko wa kimataifa wa maendeleo ya kilimo IFAD zaidi ya nusu ya watu milioni 90 wa nchi hiyo wanaishi katika maeneo yaliyoathirika vibaya na mabadiliko ya tabianchi huku wakikabiliwa na hatari kubwa ya mafuriko na wakulima ndio wanaobeba gharama kubwa ya zahma hiyo.