Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Wahudumu wa afya nchini Iran wakiangalia vifaa vya matibabu huku nchi hiyo ikiendelea kupambana na virusi vya corona.
WHO/Iran

Fedha ndio mtihani mkubwa kwa nchi kukabiliana na afya na mabadiliko ya tabianchi:WHO

Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO leo limesema nchi nyingi zimeanza kuweka kipaumbele cha afya katika juhudi zao za kuwalinda watu dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi, lakini ni takriban robo tu ya wale waliofanyiwa utafiti hivi karibuni na Shirika hilo wameweza kutekeleza kikamilifu mipango au mikakati yao ya kitaifa ya afya na mabadiliko ya tabianchi.

08 Novemba 2021

Karibu kusikiliza jarida ambapo kama ilivyo ada ya kila Jumatatu tunakuletea mada kwa kina, leo tutakuwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kuangazia ziara ya Waambata Jeshi kutoka Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, SADC ambao wanaziwakilisha nchi zao katika Umoja wa Mataifa walipozuru wilayani Beni kujionea utendaji kazi wa vikosi vya walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanaounda Brigedi ya kujibu mashambulizi FIB MONUSCO.