Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Nusu ya watu duniani watakuwa katika hatari ya mafuriko, vimbunga na Tsunami ifikapo 2030:UN
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu Tsunami Umoja wa Mataifa umeonya kwamba kufikia mwaka wa 2030, inakadiriwa kuwa asilimia 50 ya watu wote duniani wataishi katika maeneo ya pwani ambayo yanakabiliwa na mafuriko, vimbunga na tsunami.
05 Novemba 2021
Karibu kusikiliza jarida ambapo leo ni siku ya kimataifa ya uelimishaji kuhusu Tsunami, na kama ilivyo ada leo ni mada kwa kina ambapo tunaangazia vijana na mchango wao katika mabadiliko ya tabianchi wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa COP26 ukiendelea huko Glasgow Scotland.
Flora Nducha amezungumza na mmoja wa vijana wanaharakati wa mazingira kutoka nchini Kenya na mshindi wa tuzo ya shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP ya champion of the Earth 2020 kutokana na kampuni yake ya Change Makers kubadili taka za platiki kuwa tofali.
Vijana tunaweza ni wakati wa kutushirikisha kwa vitendo katika vita dhidi ya mabadiliko ya tabianchi:Nzambi
Wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP26 ukiendelea mjini Glasgow Scotland, vijana wanatoa wito kwa viongozi kutekeleza kwa vitendo ushirikishwaji wa vijana katika vita dhidi ya janga hilo.