Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Mauritania wapambana na mabadiliko ya tabianchi

siku chache kabla ya kuanza kwa mkutano huo wa 26 wa nchi wanachama wa mabadiliko ya tabianchi, ambao hivi sasa unaendelea Glascow, Scotland, Mshauri Maalumu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudunia wakimbizi, UNHCR kuhusu Hatua dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi, Andrew Harper ametembelea Mauritania kujionea jinsi wakimbizi wanavyopambana na janga la tabianchi.

(Taarifa ya John Kibego)
“Hatujawahi kuona mwaka kama 2021. Huu ni mwaka wenye mioto mingi ya nyika.” Anasema Ahmedou El-Bokhary, Rais wa Kikosi cha zima moto kinachoundwa na wakimbizi.  

Sauti
2'5"

04 Novemba 2021

Karibu kusikiliza jarida, leo ni siku ya kimataifa ya kupinga uonevu shuleni na mitandaoni ambapo UNESCO imetaka watoto kulindwa zaidi, WFP imetoa msaada kwa wananchi wa Madagascar wanaoishi katika ukame na hivyo kulazimika kula mmea wa Dungusi kakati.

Pia utasikia kauli ya Rais wa COP26 huko Glasgow kuhusu nchi tajiri kutoa fedha za kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Sauti
13'18"