Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

UN/ John Kibego

Jamii ya Watyaba kandoni mwa Ziwa Albert nchini Uganda yatishiwa tena na mafuriko

Wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP26 unaendelea katika huko Glosgow na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiwa amewaeleza viongozi wa ulimwengu kuwa ni muhimu kuchukua hatua sasa kwani wanadamu wanajichimbia kaburi, nchini Uganda jamii ya Watyaba, mojawapo ya jamii za walio wachache wanaoishi katika viunga vya Ziwa Albert, wanapaza sauti kwa serikali na shirIka  la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kuwasaidia kutokana na madhara ya mabadiliko ya tabianchi.

Sauti
3'45"

02 Novemba 2021

Leo tarehe 02 Novemba  2021 siku ya kimataifa ya kutokomeza ukwepaji sheria kwa uhalifu dhidi ya wanahabari  ASSUMPTA MASSOI anakuletea jaridi likizungumzia kwa undani juu ya siku hii na takwimu zilizotolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni,  UNESCO pamoja na ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.