Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Zaidi ya nchi 100 zimeahidi kusitisha na kubadilisha ukataji miti ifikapo 2030
Azimio la kihistoria la kuokoa na kurejesha misitu ya dunia katika ubora wake limetangazwa leo rasmi katika siku ya pili ya mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi unaoshirikisha viongozi wa dunia au COP26.
Jamii ya Watyaba kandoni mwa Ziwa Albert nchini Uganda yatishiwa tena na mafuriko
Wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP26 unaendelea katika huko Glosgow na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiwa amewaeleza viongozi wa ulimwengu kuwa ni muhimu kuchukua hatua sasa kwani wanadamu wanajichimbia kaburi, nchini Uganda jamii ya Watyaba, mojawapo ya jamii za walio wachache wanaoishi katika viunga vya Ziwa Albert, wanapaza sauti kwa serikali na shirIka la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kuwasaidia kutokana na madhara ya mabadiliko ya tabianchi.
02 Novemba 2021
Leo tarehe 02 Novemba 2021 siku ya kimataifa ya kutokomeza ukwepaji sheria kwa uhalifu dhidi ya wanahabari ASSUMPTA MASSOI anakuletea jaridi likizungumzia kwa undani juu ya siku hii na takwimu zilizotolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni, UNESCO pamoja na ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
COP26: Jamii ndogo zina mchango mkubwa katika vita dhidi ya mabadiliko ya tabianchi:Rahma Kivugo
Jamii ndogo ndogo za mashinani zina mchango mkubwa katika kusongesha ajenda ya Umoja wa Mataifa ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi amesema mmoja wa wanaharakatio wa mazingira Rahma Rashid Kivugo mratibu wa mradi wa kijamii wa Mikoko Pamoja kutoka Pwani ya Kenya.