Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Tukifanya kazi pamoja tunaweza kukabili changamoto za mabadiliko ya tabianchi:UN
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo limekutana katika mjadala wa wazi kujadili mabadiliko ya tabianchi ukijikita na mada “Utekelezaji wa hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi kwa ajili ya watu, sayari dunia na ustawi.”
Dunia bado ipo hatarini kuwa na ongezeko la joto : UNEP
Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP imeeleza kuwa ahadi mpya na zilizorekebishwa kuhusu viwango vya nchi vya kukabili mabadiliko ya tabianchi, NDCs hazijafikia lengo lililowekwa katika mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi na hivyo ulimwenguni kuwa hatarini kuwa na ongezeko la joto la angalau nyuzijoto angalau 2.7 katika karne hii
(Leah Mushi na taarifa zaidi.)
26 Oktoba 2021
Karibu usikilize jarida ambapo leo Assumpta Massoi amekuandalia habari mbalimbali zikiwemo
Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP imeeleza kuwa ahadi mpya na zilizorekebishwa kuhusu viwango vya nchi vya kukabili mabadiliko ya tabianchi, NDCs hazijafikia lengo lililowekwa katika mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi na hivyo ulimwenguni kuwa hatarini kuwa na ongezeko la joto la angalau nyuzijoto angalau 2.7 katika karne hii.