Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

ADB/Ariel Javellana
Uzalishaji kutoka kwa mitambo ya kufua umeme wa makaa ya mawe unachangia uchafuzi wa hewa huko Ulaanbaatar, Mongolia.

Uzalishaji wa mafuta ya kisukuku unapeleka kombo malengo ya mabadiliko ya tabianchi:UNEP

Licha ya kuongezeka kwa matarajio ya mabadiliko ya tabianchi na ahadi za kutokomeza kabisa uzalishaji wa hewa ukaa, serikali bado zina mpango wa kuzalisha zaidi ya mara mbili ya kiwango cha nishati kutoka kwenye mafuta ya kisukuku ifikapo mwaka 2030, kuliko kiwango ambacho kitapunguza ongezeko la joto duniani hadi kufikia kiwango kilichowekwa kwenye mkataba wa Paris cha nyuzijoto 1.5 katika kipimo cha Selsiasi (1.5° C)