Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Mabadiliko ya hali ya hewa kwa mfano ukame yanasababisha athari za kiuchumi miongoni mwa wakulima.
UN Photo/Albert Gonzalez Farran

Afrika inakabiliwa na hatari kubwa ya mabadiliko ya tabianchi:WMO

Ripoti mpya iliyotolewa leo na mashirika mbalimbali na kuratibiwa na shirika la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO imesema mabadiliko ya mifumo ya mvua, kuongezeka kwa joto na hali mbaya ya hewa kumechangia kuongezeka kwa ukosefu wa chakula, umaskini na watu kutawanywa barani Afrika mwaka 2020 huku hali mbaya ikizidishwa nachangamoto za kijamii, kiuchumi na kiafya ziliyosababishwa na janga la COVID-19.