Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Changamoto zetu haziwezi kutatuliwa kwa mtutu wa bunduki: Biden
Nguvu za kijeshi za Marekani zinapaswa kuwa ni suluhu la mwisho kutumikana sio suluhu ya kwanza, amesema Rais wa Marekani Joe Biden alipowahutubia viongozi wa dunia katika mkutano mkuu wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA76 mjini New York Marekani.
Mjadala Mkuu wa UNGA76 wafungua pazia New York
Mjadala Mkuu wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA76 leo umeng’oa nanga rasmi katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa hapa jijini New York Marekani ukifanyika moja kwa moja na pia kupitia mtandaoni ukiwaleta pamoja nchi 193 wanachama wa Umoja huo.
Flora Nducha na taarifa zaidi
Abdullah Shahid Rais wa Baraza Kuu akifungua mjadala huo ambao umebeba mada ya “Kujenga mnepo kupitia tumaini la kujikwamua kutoka kwa janga la COVID-19, kushughulikia mahitaji ya sayari dunia, kuheshimu haki za watu, na kuufufua Umoja wa Mataifa. "
Jarida 21 Septemba 2021
Leo tarehe 21 Septemba mwaka 2021 ni siku ya amani duniani halikadhalika siku ya kwanza ya mjadala mkuu wa mikutano ya ngazi ya juu ya Umoja wa Mataifa katika makao makuu ya UN nchini Marekani.
Karibu Usikilize Jarida ambapo utasikia mengi kuhusu #UNGA76
Mjadala Mkuu wa ngazi za juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa waanza rasmi
Mjadala Mkuu wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA76 leo umeng’oa nanga rasmi katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa hapa jijini New York Marekani ukifanyika moja kwa moja na pia kupitia mtandaoni ukiwaleta pamoja nchi 193 wanachama wa Umoja huo.