Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

UN Photo/Evan Schneider

Mjadala Mkuu wa UNGA76 wafungua pazia New York

Mjadala Mkuu wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA76 leo umeng’oa nanga rasmi katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa hapa jijini New York Marekani ukifanyika moja kwa moja na pia kupitia mtandaoni ukiwaleta pamoja nchi 193 wanachama wa Umoja huo.

Flora Nducha na taarifa zaidi 
Abdullah Shahid Rais wa Baraza Kuu akifungua mjadala huo ambao umebeba mada ya “Kujenga mnepo kupitia tumaini la kujikwamua kutoka kwa janga la COVID-19,  kushughulikia mahitaji ya sayari dunia, kuheshimu haki za watu, na kuufufua Umoja wa Mataifa. " 

Sauti
4'52"

Jarida 21 Septemba 2021

Leo tarehe 21 Septemba mwaka 2021 ni siku ya amani duniani halikadhalika siku ya kwanza ya mjadala mkuu wa mikutano ya ngazi ya juu ya Umoja wa Mataifa katika makao makuu ya UN nchini Marekani.
Karibu Usikilize Jarida ambapo utasikia mengi kuhusu #UNGA76

Sauti
17'16"