Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Hali ya hewa, tabianchi au majanga ya maji yanaua kwa wastani watu 115 kila siku
Maafa yanayohusiana na hali ya hewa, tabianchi au majanga ya maji yalitokea katika miaka 50 iliyopita na kuua kwa wastani watu 115 kila siku na kusababisha hasara ya dola milioni 202 kila siku, kwa mujibu wa ripoti mpya iliyotolewa hii leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa Duniani, WMO.
(Taarifa ya Moses Mghase)
Jarida Septemba 01 2021
Katika jarida na Grace Kaneiya hii leo utasikia ziara maalum ya Balozi Liberata Mulamula amaye ni waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa wa Tanzania nchi Marekani kuzungumza na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.
Pia utasikia taarifa inayoangazia ripoti mpya ya hali ya hewa iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la hali ya hewa WMO
Mabadiliko ya tabianchi yanasabisha hali mbaya zaidi ya hewa lakini maonyo ya mapema yanaokoa maisha
Maafa yanayohusiana na hali ya hewa, tabianchi au majanga ya maji yalitokea katika miaka 50 iliyopita na kuua kwa wastani watu 115 kila siku na kusababisha hasara ya dola milioni 202 kila siku, kwa mujibu wa ripoti mpya iliyotolewa hii leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa Duniani, WMO.