Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Mama akiandaa chakula kwa ajili ya binti yake kwa kutumia nafaka alizozipata kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la  mpango wa chakula, WFP, Maiduguri, Nigeria.
© WFP/Oluwaseun Oluwamuyiwa

Watu milioni 155 wanakabiliwa na njaa na kuhitaji msaada wa duniani:WFP/FAO/EU 

Idadi kubwa na inayoongezeka ya watu wanakabiliwa na njaa kali na wanahitaji msaada wa kuokoa maisha, huku idadi kubwa ya watu wenye njaa kali katika nchi zilizokumbwa na madhila 2020 ilifikia kiwango cha juu zaidi katika miaka mitano, iliyopita imesema ripoti ya kila mwaka iliyozinduliwa leo kwa pamoja na muungano wa kimataifa wa Umoja wa Mataifa, serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali yanayofanya kazi kushughulikia mgogoro wa chakula.