Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Dunia bado inaweza kutatua changamoto ya mabadiliko ya tibianchi, kutimiza SDGs na kuishi vyema na mazingira:UN
Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP inatoa muongozo wa jinsi ya kushughulikia changamoto kubwa tatu za dharura zinazoikumba dunia ambazo ni mabadiliko ya tabianchi, kuishi vyema na mazingira na ufikiaji wa malengo ya maendeleo endelevu SDGs.
18 Februari 2021
Hii leo jaridani Flora Nducha anaanza na masuala ya mazingira ambapo ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa inasema bado safari ni ndefu kukabili mabadiliko ya tabianchi. Kisha anabisha hodi Msumbiji ambako anaangazia msaada kwa manusura wa dhoruba kali Eloise. Baada ya hapo anakwenda baharí Hindi visiwani Comoro ambako mradi wa shirika la kazi duniani, ILO umeleta ajira za staha kwa wakazi maskini. Makala tunarejea tena Tanzania jijini Dar es salaam kumulika kilimo cha mboga mboga na matumizi ya muarobaini kukabili wadudu waharibifu.