Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

18 Februari 2021

Hii leo jaridani Flora Nducha anaanza na masuala ya mazingira ambapo ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa inasema bado safari ni ndefu kukabili mabadiliko ya tabianchi. Kisha anabisha hodi Msumbiji ambako anaangazia msaada kwa manusura wa dhoruba kali Eloise. Baada ya hapo anakwenda baharí Hindi visiwani Comoro ambako mradi wa shirika la kazi duniani, ILO umeleta ajira za staha kwa wakazi maskini. Makala tunarejea tena Tanzania jijini Dar es salaam kumulika kilimo cha mboga mboga na matumizi ya muarobaini kukabili wadudu waharibifu.