Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
27 Januari 2021
Hii leo jaridani Flora Nducha anaanzia nchini Tanzania kumulika harakati za watoto wa kike na elimu, kisha anakukutanisha na wajasiriamali vijana kupitia shirika la maendeleo ya viwanda la Umoja wa Mataifa, UNIDO. Baada ya hapo anakupeleka Vietnam ambako utaalamu umemaliza tabia ya wakulima kuonja maji ili kutambua iwapo yana chumvi nyingi au la kabla ya kumwagilia kwenye mpunga. Makala tunakwenda Nairobi nchini Kenya ambako kijana aliyekuwa sugu mtaani sasa amegeuka mkombozi kwa vijana wengine waliokuwa tishio mitaani na anatamatisha na mashinani kutoka Sudan Kusini, karibu!
Badala ya kuonja maji kutambua kiwango cha chumvi, sasa wakulima watumia simu ya kiganjani
Nchini Vietnam, mfuko wa maendeleo ya Umoja wa Mataifa, IFAD umesaidia wakulima kuondokana na tabia ya kuonja maji ya umwagiliaji ili kutambua kiwango cha chumvi na badala yake sasa wanatumia teknolojia ya simu ya kiganjani ili kuongeza mavuno ya mpunga